Kutoka kushoto ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta (TPB), Sabasaba
Moshingi, Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka na baadhi ya
viongozi meza kuu wakiwa wameshikana mikono na kuinyanyua juu ikiwa ni
ishara ya kuwaunganisha wastaafu kwenye fursa mara baada ya uzinduzi wa
mpango maalumu wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF
leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka akizungumza katika uzinduzi
wa mpango maalumu wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa Mfuko wa Pensheni wa
LAPF leo jijini Dar es Salaam.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi akizungumza
katika hafla ya uzinduzi wa mpango maalumu wa kutoa mikopo kwa wastaafu
wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF leo jijini Dar es Salaam.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi (kushoto)
akimkaribisha Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka meza kuu mara
baada ya waziri huyo kuzinduwa rasmi mpango maalumu wa kutoa mikopo kwa
wastaafu wa Mfuko wa Pensheni wa LAPF leo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudensia Kabaka (wa nne kulia), Ofisa
Mtendaji Mkuu wa Benki ya Posta, Sabasaba Moshingi (wa tano kulia)
wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa walioshiriki
katika mpango maalumu wa kutoa mikopo kwa wastaafu wa Mfuko wa Pensheni
wa LAPF leo jijini Dar es Salaam.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...