Balozi Celestine Mushy, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiongea jambo wakati alipokutana na wawakilishi wa nchi za G4 hapa nchini ambazo ni India, Brazil, Ujerumani na Japan. Mwingine katika picha ni Bibi Ramla Khamis, Afisa katika Wizara ya Mambo ya Nje. Balozi Mushy na wawakilishi hao walijadili masuala ya mabadiliko katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambapo alisisitiza msimamo wa bara la Afrika wa kupatiwa nafasi mbili za ujumbe wa kudumu zenye kura ya turufu katika Baraza hilo pamoja na nafasi tano za ujumbe usio wa kudumu.
Wawakilishi wa nchi za G4 nchini wakimsikiliza kwa makini Balozi Mushy hayupo pichani. kutoka kulia ni Balozi wa India nchini Tanzania, Mhe. Debnath Shaw; Naibu Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania, Mhe. John Reyels; Afisa wa Ubalozi wa Ujerumani nchini Tanzania; Naibu Balozi wa Brazil nchini Tanzania, Mhe. Pedro Martins; Afisa wa Ubalozi wa Japan nchini Tanzania, Bibi Noriko Tanaka.
Mazungumzo yakiendelea baina ya Balozi Mushy na Wawakilishi wa nchi za G4 nchini Tanzania
Picha ya Pamoja baina ya Balozi Mushy (watatu kutoka kulia) na Wawakilishi wa Nchi za G4. Picha na Anthony Guninita

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...