Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa Kata ya
Kimanzichana leo wakati alipoanza Ziara yake ya mikoa ya Pwani ,Tanga na
Iringa Ikiwa ni kuimarisha Chama na kukagua utekelezaji wa Ilani ya
Uchaguzi ya Mwaka 2010 huku akihimiza wananchi kushiriki katika shughuli
za kujiletea maendeleo katika maeneo yao, Katibu Mkuu Abdulrahman
Kinana anaongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi
na leo amefanya shughuli mbalimbali katika ziara hiyo.

Mbunge
wa jimbo la Mkuruanga na Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi Mh. Adama
Malima akizungumza na wananchi katika kijiji cha Mkuranga wakati wa
mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata hiyo leo.

Nape
Nnauye Katibu wa NEC Siasa Itikadi na Uenezi akizungumza na wananchi wa
kata ya Kimanzichana wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika mjini
hapo leo

Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga Mh. Mercy Silla akwahutubia wananchi wa kata ya Kimanzichana kwenye mkutano wa hadhara leo.

Baadhi ya wananchi
wakipunga mikono kwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo
pichani wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Kimanzichana.

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...