Mara baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Mtwara, Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 Mwanaafa Mwinzago akitoa Maneno ya Shukrani kwa Wakazi wa Mtwara waliojitokeza kuja Kumpokea uwanja wa Ndege wa Mtwara mapema Leo. Vilevile alitoa Shukrani zake zote kwa Watanzania Wote kwa Kuweza umpigia Kura na Kumfanya aibuke mshindi wa Milioni 50 za Tanzania katika fainali ya Shindano la  Kusaka vipaji vya Kuigiza lijulikanalo Kama Tanzania Movie Talents (TMT).
Wapenzi, Mashabiki na wana Mtwara wakiwa Nje ya Uwanja wa Ndege wa Mtwara wakisubiri Kumpokea Mshindi wa Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT) 2014 Mwanaafa Mwinzago kwaajili ya Kumpongeza kwa Kuibuka MShindi wa SHilingi Milioni 50 za Kitanzania katika Fainali ya Shindano la Tanzania Movie Talents (TMT)lililofanyika Mwisho wa Mwezi wa nane katika Ukumbi wa Mlimani City, Jijini Dar Es Salaam.
Wakazi wa Mkoa wa Mtwara wakimpongeza Mshindi wa TMT 2014 Mwanaafa Mwinzago ambaye amewasili Mkoani Mtwara ambapo ndio Nyumbani Kwao akitokea Dar Es Salaam mara baada ya Kuibuka Mshindi na Kujinyakulia Kitita Cha Shilingi Milioni 50 za Kitanzania.
Ndugu, Jamaa na Marafiki wa Mshindi wa TMT 2014 Mwanaafa Mwinzago wakipiga picha ya Pamoja mara baada ya Kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mtwara akitokea Dar Es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...