Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Exim Tanzania, Bw. Yogesh
Manek akishiriki zoezi la Ice Bucket Challenge kuunga mkono kampeni dhidi ya ugonjwa wa fistula nchini Tanzania, baada
ya kuteuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, Sunil Colaso. Tukio
hilo lilifanyika katika ofisi za makao makuu ya benki hiyo mwishoni mwa wiki
jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Exim Tanzania, Bw. Yogesh
Manek akizungumza na waandishi kabla kushiriki zoezi la Ice Bucket Challenge kuunga mkono kampeni dhidi ya ugonjwa wa fistula nchini Tanzania, baada
ya kuteuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, Sunil Colaso. Tukio
hilo lilifanyika katika ofisi za makao makuu ya benki hiyo mwishoni mwa wiki
jijini Dar es Salaam.
======== ====== =========
Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya Exim Tanzania,
Bw. Yogesh Manek ameshiriki katika Ice Bucket Challenge, kuunga mkono kampeni
dhidi ya ugonjwa wa fistula nchini Tanzania, baada ya kuteuliwa na Mkurugenzi
Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, Sunil Colaso.
Kabla ya kumwagiwa maji yenye barafu Bw.
Manek aliwateua, Ali Mafuruki Mwenyekiti na Afisa Mtendaji Mkuu wa Infotech
Investment Group, Shabir Abji, Mwenyekiti wa Hotel ya New Africa na Veena Jog, Mkurugenzi
Mtendaji wa Advent Constructions Ltd kushiriki katika zoezi hilo ikiwa ni
jitihada za kuwaokoa wanawake wakitanzania wenye tatizo la ugonjwa huo wa
fistula.
Akizungumza kabla ya kushiriki,
Jumapili, Bw. Yogesh Manek alisema amehamasika kukubali shindano hilo kutokana
na idadi kubwa ya maisha inayopotea na ulemavu unaosababishwa na ugonjwa huo:
pamoja na zoezi hilo kunakshiwa na mpango wa utunzanji mazingira wa benki hiyo
ujulikanao kama ‘Exim Go Green’ Maji kwa matumizi mazuri.
“Namshukuru Bw. Sunil Colaso,
Mkurugenzi wa Airtel Tanzania, kwa kunichagua kufanya zoezi hili ambalo
nimelipokea kwa heshima kubwa sababu nafahamu urishiriki wangu utaukoa maisha ya
walio wengi na kusaidia Tanzania kuwa huru dhidi ya fistula. Kwa mujibu wa
takwimu zilizopo zaidi ya wanawake 8000 ufariki kutokana na fistula, 160,000
upata ulemavu na zaidi ya watoto 40,000 wa chini ya mwaka mmoja ufariki
kutokana na ugonjwa huu unaotibika,” alisema.
Alibainisha kuwa Benki ya Exim,
imekuwa ni katika mstari wa mbele kuunga mkono shughuli mbali mbali zenye
manufaa kwa wanawake, ndiyo maana kampeni ya fistula imekuja kwa wakati
muafaka.
“Benki ya Exim imekuwa ikiunga mkono
miradi mbali mbali ya kimaendeleo ya kijamii, hususani katika sekta za afya,
mazingira na elimu.
“Hii imethibitishwa na baadhi ya
shughuli za kijamii tulizofanya hivi karibuni, ikiwa ni pamoja na kuchangia
magodoro katika hospitali ya Mwananyamala, kuijengea shule ya msingi Kilakala
vyoo na kushiriki kikamirifu katika shughuli za usafi wa mazingira nchi nzima,
ili kuwa na mazingira safi.
“Na leo hii, ninashiriki katika Ice
Bucket Challenge kuonyesha jitihada zetu kama benki katika kuendelea kuunga
mkono shughuli hizo,” alisema Bw. Manek. Alisema kuwa wafanyakazi wote wa
Benki ya Exim wameunga mkono zoezi hili la Ice Bucket Challenge ambalo
limeanzishwa kwa lengo zuri.
“Tunafuraha
kubwa na kiwango cha huruma, ukarimu na hisia zilizoonyeshwa na wafanyakazi
wote, wao pia wakishiriki katika zoezi hili muhimu kikamirifu," alisema Bw
Manek.
Bw. Manek
alibainisha pia, zoezi hilo pia limelenga katika kukuza ushiriki wa wafanyakazi
na watu wengine katika shughuli za kijamii ambazo benki imekuwa ikianzisha mara
kwa mara ikiwa na lengo la kusaidia kukuza sekta mbali mbali za kiuchumi na
kijamii nchini.
Benki ya Exim ni moja kati ya benki
kubwa nchini kwa upande wa mali zake za jumla, na kuwa na matawi 32 nchi nzima
ikisambaa katika uchumi wa nchi tatu Afrika.
Uncle Shikamoo. Ombi langu ni kuomba matangazo kama haya,mtuwekee jinsi gani watu wa ughaibuni wanaoweza kuchangia,wakapata njia za mawasiliano na ofisi husika
ReplyDelete