Katibu Mkuu wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia,Mh.Jonh Mgodo akizungumza mapema leo mbele ya Wanahabari kuhusiana na uzinduzi wa Programu mpya ya kujifunza somo la hisabati kwa kutumia simu za mikononi.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia,Mh.Jonh Mgodo akizungumza mapema leo mbele ya Wanahabari katika ukumbi wa COSTECH,Sayansi Kijitonyama,jijini Dar kuhusiana na uzinduzi wa Programu mpya ya kujifunza somo la hisabati kwa kutumia simu ya mikononi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Sayansi na Teknolojia,Mh.Jonh Mgodo (wa tatu shoto) akioneshwa na mmoja wa wataalamuwa programu hiyo mpya ya kujifunza somo la hisabati kwa kutumia simu ya mikononi,iliyozinduliwa leo inavyoweza kufanya kazi katika simu za mikononi.
 Mmoja wa Wataalamu wa mradi huo wa Programu mpya ya kujifunza somo la hisabati kwa kutumia simu za mikononi,kutoka Nokia Mobile Mathematics,Bi.Riita Vanska akifafanua jambo kwa wanahabari na wageni waalikwa mbalimbali waliofika kwenye hafla hiyo iliyofanyika leo katika ukumbi wa COSTECH,Sayansi Kijitonyama,jijini Dar.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia  COSTECH,Dkt.Hassan Mshinda ambao pia ni sehemu ya mafanikio ya programu hiyo,akizungumza jambo mbele ya wanahabari (hawapo pichani) kuhusiana na uzinduzi wa programu mpya ya kujifunza somo la hisabati kwa kutumia simu za mikononi. 
  Baadhi ya wageni waalikwa na wadau mbalimbali wakiwa kwenye hafla hiyo wakifuatilia kwa makini yaliyokuwa yakijiri ukumbini humo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Inaonekana inaweza kuwa programmu nzuri inayoweza kuwafikia wengi kwa simu za mkononi.

    ReplyDelete
  2. Kwa Masomo Yote ya Sayansi for Android OS, Programmu hizi hapa (free)

    Mathematics (O-level): https://play.google.com/store/apps/details?id=com.myexample.MyMath_TZ

    Physics(O-level): https://play.google.com/store/apps/details?id=com.myexample.Physics_TZ

    Chemistry(O-level): https://play.google.com/store/apps/details?id=com.myexample.Chemistry_TZ

    Biology(O-level): https://play.google.com/store/apps/details?id=com.myexample.o_level_biology

    Mathematics (KCSE): https://play.google.com/store/apps/details?id=com.myexample.kcse_kenya_math

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...