Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa masikitiko kifo cha mwamuzi wa daraja la kwanza (class one), Luteni  David Lugenge kilichotokea jana (Septemba 7 mwaka huu) kwa ajali ya gari katika Wilaya ya Handeni mkoani Tanga.

Luteni Lugenge ambaye mwishoni mwa wiki alishiriki mitihani ya utimamu wa mwili kwa waamuzi wa Ligi Kuu alikuwa na ndugu yake Christopher Alexander Lunyungu katika gari dogo wakienda mkoani Kilimanjaro.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Handeni, Peter Juma, Luteni Lugenge alikuwa akimsindikiza mwenzake aliyekuwa anakwenda kujitambulisha kwa wakwe zake watarajiwa.

Msiba huo ni mkubwa katika familia ya mpira wa miguu kwani Luteni Lugenge alikuwa ni mmoja wa waamuzi wanaoinukia nchini, hivyo mchango wake ulikuwa bado unahitajika. Hivyo tutamkumbuka daima.

TFF tunatoa pole kwa familia ya marehemu Luteni Lugenge, Chama cha Waamuzi wa Mpira wa Miguu nchini (FRAT) na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na kuwataka kuwa na subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito.

BONIFACE WAMBURA
KNY KATIBU MKUU

SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...