Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Bw. Eliya Ntandu akifungua mafunzo ya siku sita ya maofisa watakaoshiriki katika Tathmini ya kina ya Matukio Muhimu ya Mwanadamu. Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Shughuli za Kitakwimu wa NBS, Bi Aldegunda Komba, Mkurugenzi Mkuu wa NBS, Dk. Albina Chuwa, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Bi Emmy Hudson na Kamishna wa Sensa, Hajjat Amina Mrisho Said.
 Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Bi. Emmy Hudson akitoa maelezo kuhusu ushiriki wa RITA katika tathmini.
 Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu, Dk. Albina Chuwa akitoa maelezo kuhusu ushiriki wa NBS katika tathmini.
Picha ya Mgeni Rasmi na washirki wa Mafunzo.

Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA) kwa kushirikiana na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) wanaendesha mafunzo ya siku sita kwa maofisa watakaoshirki kufanya tathmini ya kina ya Usajili na Takwimu za matukio muhimu ya mwanadamu ambayo ni Vizazi, Vifo, Ndoa na talaka. Mafunzo hayo yamefunguliwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Bw. Eliya Ntandu Jana Jumanne tarehe 2 Septemba 2014 na yanafanyika katika ukumbi wa 88 Motel, Mkoani Morogoro.

Mafunzo hayo yanawashirikisha maofisa kutoka taasisi mbali mbali zinazohusika na masuala ya usajili wa wananchi ikiwa ni maandalizi kwa ajili ya kuwapa uwezo wa kufanya tathmini ya kina ya mifumo na sheria zilizopo zinazohusika na usajili wa matukio muhimu ya mwanadamu ambayo ni Vizazi, vifo, Ndoa na Talaka .

 Tathmini inategemewa kufanyika tarehe 15 -30 Septemba 2014 katika mikoa na wilaya mbalimbali nchini na maofisa waliopewa mafunzo wataweza kukusanya taarifa katika vituo vya tiba, vituo vya polisi, ofisi za wasajili wa wilaya, ofisi za kata, nyumba za ibada na katika makazi ya wananchi.

 Matokeo ya Tathmini yanategemewa kutoa mwelekeo katika mchakato wa kuweka vipaumbele na mipango ya utekelezaji wa mfumo thabiti wa usajili wa raia na utoaji wa takwimu za matukio muhimu, mfumo utakaokuwa kiungo muhimu katika utekelezaji wa utawala bora na pia chanzo cha msingi cha takwimu za matukio kama vizazi, ndoa, talaka na vifo na sababu zake.

RITA NA NBS wanafanya tathimini hii ikiwa ni utekelezaji wa moja ya maazimio ya  Mkutano Mawaziri wanaohusika na masuala ya usajili wa raia wa nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika Mwaka 2012 katika Jiji la Duban, Afrika ya Kusini. Kwa mujibu wa azimio hilo kila nchi mwanachama inatakiwa kufanya tathmini hii na kuwasilisha matokeo yake katika kikao kama hicho kinachotegemewa kufanyika  mwanzoni mwa mwaka ujao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...