Kaimu Kamishna wa Madini, Mhandisi Ally Samaje akiwakaribisha wajumbe wa mkutano wa kujadili ushirikishwaji wazawa (local content) katika sekta ya madini uliofanyika jijini Mwanza hivi karibuni. Waliokaa meza kuu kutoka kushoto ni Kamishna Msaidizi Kitengo cha Uchumi na Biashara, Salim Salim, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Ndalo Kulwijila na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, John Henjewele.
Mwanasheria wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) Rose Mponguliana akiwasilisha mada kuhusu uwajibikaji wa Shirika hilo katika suala la ushirikishwaji wazawa wakati wa mkutano baina ya Serikali na Makampuni ya Madini uliofanyika hivi karibuni jijini Mwanza.
Wajumbe wa Mkutano baina ya Serikali na Makampuni ya Madini uliojadili ushirikishwaji wazawa katika sekta ya madini wakisikiliza hotuba ya Mgeni Rasmi, Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Ndalo Kulwijila (hayupo pichani).
Wajumbe wa Mkutano baina ya Serikali na Makampuni ya Madini uliojadili ushirikishwaji wazawa katika sekta ya madini wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo katika Hoteli ya Gold Crest jijini Mwanza hivi karibuni. Kutoka Kushoto waliokaa ni Kaimu Kamishna Msaidizi wa Madini Sehemu ya Uongezaji Thamani Madini Latifa Mtoro, Kaimu Kamishna wa Madini, Mhandisi Ally Samaje, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndalo Kulwijila na Mkuu wa Wilaya ya Tarime, John Henjewele.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...