Shiriko
lisilo la Kiserikali la Farm Africa kwa kushirikiana na wakulima wa
uyoga wa wilaya za Mbulu na Babati wiki iliyopita waliandaa siku maalum
ya kula uyoga kwa wakazi wa wilaya hizo.
Tukio
hilo lilifanyika katika katika kitongoji cha Magugu wilayani Babati
ambapo wakazi walipata nafasi ya kuonja aina mbalimbali za mapishi ya
uyoga.Wakulima 15 wa uyoga walio katika mradi wa Misitu wa Farm Africa
walishiriki shughuli hiyo kwa kupika na kugawa bure uyoga uliopikwa kwa
wakazi wa eneo hilo.
Kilimo
cha uyoga ni njia mbadala iliyopo kwenye mradi wa misitu ambapo
wakulima badala ya kukata miti kwa ajili ya kuitumia kwa kuwapatia
kipato, wanapanda uyoga ambao wanauuza na kuwaingizia kipato.
Siku
ya kuonja uyoga ilikuwa na madhumuni ya kuwahamasisha wakazi wa Babati
kuhusu faida za kilimo cha uyoga, mapishi yake na jinsi kilimo hicho
kinavyoweza kuwaingizia kipato cha ziada.
Ni wakati wa kula uyoga!
Wadau wakipatiwa mafunzo ya kilimo cha uyoga na wakulima walio kwenye mradi wa misitu wa Farm Africa
Wakulima wakionyesha jinsi uyoga unavyooteshwa
Wananchi wakiburudika na rosti ya uyoga
Wananchi wakipakuliwa rosti ya uyoga.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...