Marehemu Dr. Habiba Muza Rajabu wakati wa uhai wake.

Familia ya Marehemu Mzee Iddi Rajabu Mtoro wa Utemini, Singida inasikitika kutangaza kifo cha Dr. Habiba Muza Rajabu kilichotokea siku ya Jumamosi tarehe 27 Septemba 2014 hapa katika mji wa Trondheim, Norway.

Msiba uko Utemini, Singida na hapa Trondheim, Norway.

Dr. Habiba Muza Rajabu alishawahi kuwa Mhadhiri (Lecturer) katika Idara ya Chemistry, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Dr. Habiba Muza Rajabu atazikwa hapa katika mji wa Trondheim, Norway siku ya Jumatano, 1 Octoba 2014 majira ya saa 7 mchana katika eneo la Svanholm Hallen at Moholt. Kumuaga kuanzia saa 7 mchana hadi saa 7:45. Baada ya hapo maziko ya Kiislam yatafanyika hapo hapo.

INALILAHI WAINA ILAHII RAJUUN (HAKIKA SISI SOTE NI WA MWENYEZI MUNGU NA KWAKE TUTAREJEA)

Imetangazwa na: Rajabu Iddi Rajabu,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Inna lihah waina illahi rajuun. Pole Mshuwa tulikuwa pamoja METU!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...