Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (wa nne kushoto)
akipeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya WENTWORTH
inayochimba gesi katika eneo la Mnazi Bay Mkoani Mtwara , Robert MacBean
(wa tatu kushoto) mara baada ya kusaini Makubaliano ya Mkataba wa Kuuziana
Gesi kati yake na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC). Wengine katika
picha ni baadhi wa Watendaji Wakuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Shirika la
maendeleo ya Petroli Tanzania TPDC na wawakilishi wa kampuni za WENTWORTH
na MAUREL & PROM.
Wajumbe waliohudhuria kikao cha Kusaini Mkataba wa Kuuziana Gesi kati ya
Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), na Kampuni zinazochimba gesi
katika eneo la Mnazi Bay Mkoani Mtwara za WENTWORTH Resources Limited na
MAUREL & PROM wakisaini MKataba huo. Anayeshuhudia mbele ni Waziri wa
Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo pamoja na wawakilishi wengine
kutoka kampuni hizo, TPDC, Wizara ya Nishati na Madini na Shirika la Umeme
Tanzania (TANESCO).
Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) James
Andilile (wa kwanza kulia) wakipitia Mkataba kwa pamoja na mmoja wa
wawakilishi wa Kampuni hizo wakati wa kusaini Mkataba huo. Katikati ni
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya MAUREL & PROM, Michael Hochard na wa
kwanza ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya WENTWORTH Robert MacBean.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...