Katibu wa Baraza kuu la Waisalam Mkoa wa Lindi (BAKWATA) Alhaj Abdillah
Salum akifunga mafunzo kwa viongozi wa Kiislam pamoja na waalim wa
madrasa katika Manispaa ya Lindi kuhusiana na Vita dhidi ya VVU/UKIMWI
Chini ya Uwezeshaji wa AMREF kwa Ufadhili wa Global Fund.
viongozi wa dini ya kiislam wakipata mafunzo toka kwa mkufunzi wa mafunzo hayo,sheikh Shomari Mchongoma.
Maelezo ya Semina hiyo.
Na ABDULAZIZ ,Globu ya Jamii - Lindi
Viongozi wa dini mkoani Lindi wameaswa kuhimiza maadili mema kwa
waumini wao ili kukabiliana na mmomonyoko wa maadili unaosababisha
jamii kutenda matendo maovu ikiwemo kupiga vita ongezeko la maambukizi
ya VVU na Ukimwi miongoni mwa jamii.
Wito huo ulitolewa na Katibu wa Baraza kuu la waislam (BAKWATA)Mkoa wa
Lindi,Alhaj Abdillah Salum alipokuwa akifunga mafunzo ya elimu ya
Kupambana na maambukizi ya VVU na UKIMWI kwa kwa waalim wa
madrasa,Maimamu pamoja na viongozi wa Dini upande wa akina mama wa
Manispaa ya Lindi.
Mafunzo Hayo ya jinsi ya kukabiliana na kuepuka maambukizi ya ukimwi
kwa viongozi wa dini ya kiislam wa wilaya ya Lindi mjini yaliyofanyika
mjini Lindi chini Usimamizi wa AMREF kwa Ufadhili wa Global Fund
yameshirikisha jumla ya washiriki 50 na kuendeshwa na kitengo cha
Ukimwi Bakwata Taifa(BAK-AIDS).
Alhaj Abdillah Salum alibainisha kuwa mafunzo hayo Yanatolewa kupitia
Viongozi hao ili wasaidie kuirekebisha jamii kutoka kwenye mmomonyoko
wa maadili unaosababisha itende maovu.
Masheikh zangu Kitengo cha ukimwi makao makuu kimeona ni vema kuwapa
elimu hii kwa kuwa munayo nafasi kubwa kutokana na kuwa na wafuasi
wengi mnaoweza kuwafikishia ujumbe kwa wakati kupitia maeneo ya Ibada
na mafundisho ya Dini ili kuhakikisha VVU na Ukimwi inatokomea katika
mkoa wetu....alimalizia Alhaj Salum.
Kwa upande wake mkufunzi wa masuala ya Ukimwi kitengo cha
UKimwi,BAKWATA makao makuu,Shomari Mchongoma alisema mmomonyoko wa
maadili unashamiri kutokana na wenye wajibu wa kuielimisha jamii
kuacha kutimiza wao na kugeuka kuwa walalamikaji.
"Ongezeko la watoto
wa mitaani ni matokeo ya wanaositahili kuielimisha jamii kupitia
nafasi zao kukwepa jukumu hilo na kuishia kulalamika Hivyo viongozi wa
dini tunalojukumu kubwa la kufikisha mahubiri kwa waumini wetu,ikiwamo
namna ya kuepuka maambukizo ya Ukimwi hivyo jambo hili sio la
kuiachia serikali peke yake"alisema Mchongoma.
Mafunzo hayo ya siku tatu ambayo yanafadhiliwa na AMREF yanalenga
kuwajengea uwezo kwa viongozi hao wa dini ili kutambua mbinu za
kukabiliana na maambu kizo ya UKIMWI yalifunguliwa na Mkuu wa wilaya
ya Lindi Dr Nassor Ally Hamid yakisimamiwa na Hamis Mayunga Afisa
Tathmini Bakwata Makao Makuu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...