Mshindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 Gerald Kitabu
(The Guardian) akisalimiana na kijana wa Kizulu katika kijiji
cha Utamaduni cha Lesedi walipotembelea ili kujifunza utalii wa
kiutamaduni nchini Afrika Kusini.
Mshindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 Vedasto
Msungu (ITV) akisalimiana na kijana wa Kizulu katika kijiji cha
Utamaduni cha Lesedi walipotembelea ili kujifunza utalii wa
kiutamaduni nchini Afrika Kusini.
Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 kutoka kulia
Gerald Kitabu, David Rwenyagira na Vedasto Msungu wakifurahi
pamoja na wanakijiji cha Wazulu cha Lesedi walipowatembelea ili
kujifunza utamaduni wao.
Mshindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 David Rwenyagira
(Radio Five) akishika ngao kwa ajili ya kujikinga na adui ambao ni
mojawapo ya utamaduni wa Wazulu.
Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 wakiendelea
kupata somo juu ya tamaduni mbalimbali zinaopatikana nchini
Afrika Kusini.
Washindi wa Tuzo za Habari za TANAPA 2013 katika picha ya
pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Kituo cha Utamaduni cha
Lesedi, Afrika Kusini.
Lugha ya Kiswahili nayo yafahamika vema Afrika Kusini kama
inavyoonekana hapa katika picha iliyopigwa na Washindi wa Tuzo
za Habari za TANAPA 2013.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...