Taasisi isiyo ya kiserikali ya MAYEPS Tanzania imezindua kitabu kiitwacho “NITUNZE NIKUTUNZE FAINALI UZEENI”, chenye maudhui ya kuwasaidia watu wanaofanyakazi ya kujiajiri au kuajiriwa kufanya maamuzi yaliyosahihi ili waweze kuishi maisha bora wakati wakiwa kwenye ajira na baada ya kustaafu.

Akizungumza na waandishi wa habari hivi karibuni jijini Dar es salaam, Meneja wa Taasisi hiyo John Masumba amesema kuwa uzoefu unaonesha kuwa wafanyakazi katika jamii ya Kitanzania hawaweki akiba kwa ajili ya kuwekeza kwa madhumuni ya kujenga uchumi. 

Meneja Masumba amesisitiza kuwa MAYEPS imetambua kwamba ikiandaa warsha moja kwa mwezi juu wafanyakazi kufanya maamuzi yaliyo sahihi, itawafikia watu 600 kwa mwaka.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Rose Mang’enya aliwapitisha waandishi wa habari juu ya yaliyomo kwenye kitabu hicho kwa kuendesha warsha fupi iliyowafungua macho waandishi hao kuhusu namna ya kutunza fedha kuandaa maisha ya baadaye. 

Akinukuu kauli ya mtaalamu wa uongozi John Maxwell Mwenyekiti huyo alisema kuwa “Watu wanaofanikiwa na wasiofanikiwa hawatofautiani sana kiuwezo bali wanatofautiana katika dhamira ya kufika kilele au upeo wa  uwezo wao”.
Mang’enya aliongeza kuwa jukumu la kujenga maisha  binafsi   lipo kwa muhusika binafsi, hivyo, watumishi wawe na msimamo sahihi utakaowawezesha kuwa na maisha bora.

Aidha, MAYEPS hutoa mafunzo  kwa wafanyakazi wa Umama na binafsi namna ya kupanga matumizi.  Pia hutoa  mafunzo  ambayo yatawezesha wafanyakazi kutambua kuwa fedha za mafao au pensheni hupungua thamani mwaka hadi mwaka hivyo uwekezaji wa fedha hizo ni muhimu ufanywe kwa uangalifu.
 Mwezeshaji wa Taasisi ya MAYEPS Tanzania Lucas Marco (kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) hivi karibuni jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa kitabu kiitwacho “NITUNZE NIKUTUNZE FAINALI UZEENI”, chenye maudhui ya kuwasaidia watu wanaofanyakazi ya kujiajiri au kuajiriwa kufanya maamuzi yaliyosahihi ili waweze kuishi maisha bora wakati wakiwa kwenye ajira na baada ya kustaafu. Katikati ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo Rose Mang’enya na kushoto ni Meneja wa Taasisi hiyo John Masumba.
1 Mwezeshaji wa Taasisi ya MAYEPS Tanzania Lucas Marco (wa pili kulia) akimpongeza Mwenyekiti wa Taasisi ya MAYEPS Tanzania Rose Mang’enya wakati wa uzinduzi wa kitabu kiitwacho “NITUNZE NIKUTUNZE FAINALI UZEENI” hivi karibuni jijini Dar es salaam. Wa kwanza kushoto ni Meneja wa Taasisi hiyo John Masumba na Afisa Habari Idara ya Habari MAELEZO Eleuteri mangi (kulia). (Picha na MAELEZO).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mayeps Hongereni sana!

    Watanzania tumedumaa sana ktk suala la kuweka akiba, watu wakiishi maisha ya ponda mali kufa kwaja wakati huohuo (endapo je kama ukiwa umefikia uzeeni hujakufa je itakuwaje?) kwani tukumbuke ya kuwa pia vilevile Fainali Uzeeni!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...