Aliyeshika karatasi ni Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji Mhe. Dr. Mary Michael Nagu akibainisha fursa mbalimbali za Uwekezaji zilizo Tanzania. Akihutubia Wafanyabiashara hao amewashauri kuchangamkia fursa mbalimbali katika sekta za kilimo, gesi, utalii, madini na ujenzi. Kongamano la Biashara limeandaliwa na Ubalozi wa Tanzania Ubelgiji kwa kushirikiana na Taasisi ya Biashara ya Ubelgiji na Luxembourg.
Pichani ni sehemu ya Wafanyabiashara wa Ubelgiji na Luxembourg wakimsikiliza Mhe. Dr. Mary Michael Nagu Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji. Mhe. Nagu amehutubia Wafanyabiashara hao leo hii Brussels kwenye Kongamano la Biashara lililoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania Ubelgiji kwa kushirikiana na taasisi ya Biashara ya Ubelgiji.
Waziri wa Uwekezaji na Uwezeshaji Dr. Mary Michael Nagu (wa pili kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi wa Tanzania Ubelgiji Dr. Diodorus Buberwa Kaamala (wa kwanza kulia) na Bwana Maurice Vermeesch Mwenyekiti wa Taasisi ya Wafanyabiashara wa Ubelgiji. Wa kwanza kushoto ni Bwana Christopher Mramba Msaidizi wa Mhe. Nagu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...