Na John Gagarini, Kibaha
HUKU ikiwa imepita wiki moja ya tukio ambalo lilisababisha kifo cha mfanyabiashara wa Jijini Dar es Salaam  Mahoro Mlelwa kupigwa risasi na majambazi na kufa eneo la Maili Moja wilayani Kibaha watu wanaodhaniwa kuwa ni wezi wakiwa na silaha za jadi wamevamia maduka na kupora.

Watu hao walivamia maduka hayo baada ya kupiga baruti kwa lengo la kuwatisha watu ili waweze kufanikisha wizi huo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana mjini Kibaha kaimu kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Athuman Mwambalaswa (pichani) alisema kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 26 mwaka huu majira ya saa 2 usiku.
Kamanda Mwambalaswa alisema kuwa mawili yaliyopo eneo la Kwa Mathias wilayani Kibaha na kufanikiwa kupora fedha taslimu kiasi cha shilingi 200,000 pamoja na simu 4 pamoja na vocha za simu zenye thamani ya shilingi 200,000.
“Katika tukio hilo watu hao walivamia kwa Godfrey Lunyelele (32) na kumwibia simu nne na fedha taslimu kiasi cha shilingi 100,000 na kwa Hassan Mkuwili (42) waliiba vocha za simu zenye thamani ya shilingi 200,000 na fedha taslimu shilingi 100,000,” alisema Kamanda Mwambalaswa.
Aidha alisema Lunyelele alipata ujasiri baada ya kubaini silaha hizo hazina madhara na kumpiga kwa tofali kichwani mwizi mmoja kati ya watatu, na alipoanguka chini walimkamata na anashikiliwa na jeshi hilo kuhusiana na tukio hilo.
“Mtu tuliyemkamata jina linahifadhiwa ili uchunguzi usiharibike na tunaendelea kumshikilia ili atupe taarifa za wenzake ambao walifanikiwa kukimbia,” alisema Kamanda Mwambalaswa.
Alibainisha kuwa kutokana na tukio hilo wamefanya kikao na maofisa wa jeshi hilo na kuamua kufanya doria ya nguvu ya miguu pamoja na magari ili kuhakikisha wanafanikiwa kudhibiti matukio hayo na kuwataka wananchi kutoa taarifa ya watu wanaowadhania kuwa ni majambazi.
Mwisho. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...