Na Abdulaziz Ahmed, Lindi
Watu wawili wamekufa na wawili kujeruhiwa baada ya gari waliyokuwa wanasafiria kuacha njia na kupinduka katika kijiji cha Michenga, wilaya ya Ruangwa Ruangwa mkoani Lindi.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Lindi, ACP Renatha Mzinga alisema gari hiyo aina ya Toyota Rava4 yenye namba za usaji T574CWC.Iliyokuwa inaendeshwa na Mohamed Mchalaganya(27) iliacha njia na kupinduka katika barabara ya Ruangwa-Nanganga, ilitokea jana saa 11.30 jioni.

Kamanda Mzinga aliwataja waliokufa kwenye ajali hiyo kuwa ni Binasa Mapua(51) mkazi wa Tabata Dar-eS-salaam na Elizabeth Chipoleka(53),mkazi wa Yombo, Dar es salaam.

Kamanda Mzinga amewataja waliojeruhiwa kuwa ni Mussa Mchalanganya na Rashid Mchalanganya ambaye ni mwanafunzi katika Chuo cha Usafirishaji (NIT), ambapo wote ni wakaazi wa Tabata, Dar es salaam. Dereva wa gari hilo ametiwa mbaroni na upelelezi unaendelea kujua chanzo hasa cha ajali hio.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Inasikitisha watu wanapoteza maisha na gari linageuke kuwa kitu kingine kilichogongwa gongwa.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...