Balozi wa Tanzania Ubelgiji Dr. Diodorus Buberwa Kamala akimkabidhi Mkurugenzi wa Afrika wa kampuni ya TE (TE Connectivity) Bi. Patricia Testa kitabu kinachobainisha fursa za uwekezaji Tanzania. Bi. Patricia amemtembelea Balozi Kamala leo Ofisi kwake Brussels kumweleza mipango ya kampuni yake kuingia katika soko la Tanzania. Pamoja na mambo mengine Balozi Kamala ameishauri kampuni hiyo kushiriki ziara ya Wafanyabiashara na Wawekezaji wa Ubelgiji itakayofanyika Tanzania mwezi Novemba mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...