Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) akizungumza na Uongozi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) wakati alipotembelea ujenzi wa Daraja la Kigamboni,jijini Dar es Salaam leo.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) akipokea kadi maalum ya pongezi ya siku yake ya kuzaliwa leo Oktoba 07,2014 kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dkt. Ramadhan Dau.Rais Kikwete anasherehekea siku yake ya kuzaliwa leo,akiwa ametimiza miaka 64 toka kuzaliwa kwake.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiangaliwa maendeleo ya ujenzi wa Daraja Kigamboni jijini Dar es Saalam leo,wakati alipotembelea kuona maendeleo yake.
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alieambatana na Waziri wa Ujenzi,Dkt. John Magufuli,Waziri wa Kazi na Ajira,Mh. Gaudencia Kabaka na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Mh. Said Meck Sadick wakitembelea eneo la Mradi wa Ujenzi wa Daraja la Kigamboni jijini Dar es Salaam leo.ujenzi huo unafanywa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...