JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA FEDHA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
KUIMARIKA
KWA MFUMO WA KUDHIBITI FEDHA HARAMU
Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ni mwanachama mwanzilishi wa Umoja wa Nchi za Mashariki
na Kusini mwa Afrika wa Kudhibiti Fedha Haramu (The Eastern and Southern Africa
Anti - Money Laundering Group (ESAAMLG)) ulioanzishwa mwaka 1999, kwa lengo la kuweka mikakati ya pamoja ya
kudhibiti fedha haramu na ufadhili wa ugaidi kwa nchi za Mashariki na Kusini
mwa Afrika. Baada ya kuanzishwa kwa
umoja huo, Tanzania ilitunga Sheria za Kudhibiti Fedha Haramu mwaka 2006.
Umoja
wa ESAAMLG umejiwekea utaratibu wa
kufanya tathmini ya mifumo yao ya kudhibiti fedha haramu na ufadhili wa ugaidi
kwa kuzingatia mazingira ya nchi wanachama na viwango vya kimataifa
vilivyowekwa na kikosi kazi cha kimataifa kijulikanacho kama “The
Financial Action Task Force “(FATF)”.
Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ilifanyiwa tathmini ya mfumo wake wa kudhibiti fedha
haramu na ufadhili wa ugaidi mwaka 2009.
Tathmini hii ilihusu maeneo ya kisheria, sera na kitaasisi. Aidha, mkutano wa FATF uliofanyika mwezi
Juni, 2014 mjini Paris - Ufaransa, ulijadili hatua mbalimbali zilizochukuliwa
na Tanzania na kuridhika kuwa hatua hizo ni kubwa na endelevu na kuwa ipo dhamira ya hali ya juu ya kisiasa
katika kuimarisha mfumo wa kudhibiti fedha haramu na ufadhili wa ugaidi nchini.
Pamoja
na hatua hizi muhimu za kuimarisha mfumo wa kudhibiti fedha haramu na uhalifu
kwa ujumla, Kitengo chetu cha Kudhibiti Fedha Haramu kimekua mwanachama wa
umoja wa vitengo vya kudhibiti fedha haramu duniani unaojulikana kama “Egmont Group of Financial Intelligence
Units”. Kujiunga na umoja huu kutakiwezesha kitengo cha kudhibiti Fedha
Haramu Tanzania kuimarisha ushirikiano na
taasisi zinazoshughulikia udhibiti wa fedha haramu na ufadhili wa ugaidi
duniani, kurahisisha kupata taarifa za kiintelijensia zinazotakiwa katika
utendaji wake wa kazi na kuongeza weledi na tija ya utendaji kazi kupitia
mafunzo maalum na ubadilishanaji utaalam baina ya vitengo vya udhibiti wa fedha
haramu.
Kutokana
na hatua zote hizi, tunapenda kuujulisha umma kuwa, Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania imeingizwa katika orodha ya nchi zenye mifumo imara ya Kudhibiti Fedha
Haramu na Ufadhili wa Ugaidi na hivyo tutaendelea kuimarisha na kusimamia mfumo
wetu kwa manufaa na usalama wa mali za wananchi wetu.
Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania bila fedha haramu wala uhalifu inawezekana!!
Taarifa hii imetolewa na
Katibu Mkuu
Wizara ya Fedha
11468 Dar Es Salaam
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...