Na Sultani Kipingo
Yaani ni kama kwamba kubadilika kimchezo kwa kipa wa Man U David de Gea kutoka kuwa mchekea
hadi mmoja wa makipa bora wa ligi kuu ya Uingereza kumekamilika. De Gea, hapana
shaka, leo amedhihirisha kuwa mmoja wa walinda mlango hodari, tofauti na na
msimu uliopita alipookuwa chini ya kocha David Moyes. Leo Mhispania huyu
ameokoa penati na kupangua mipira kibao kumyima Mzee Arsene Wenge na Arsenal
yake pointi 2 na kumuokoa kocha mpya Louis van Gaal kutoka katika kuti kavu
Ngoma ilikuwa nzito toka kipyenga cha
kwanza. Ulikuja pale Cesc Fabregas alipotoa pande tamu kwa Diego
Costa ambae alipiga bao moja tamu sana. Kofi la uso kwa mashabiki walioanza
kumbeza. Hata hivyo jambo ambalo lingempa hofu Wenger na timu zote zingine ni
kwamba leo Chelsea wametandaza kabumbu lisilo la kawaida, na kuhakikisha kuwa
hio sio timu ya mtu mmoja. Naam, Costa alifunga tena, lakini hakuwa akihitajika
sana. Maana ngoma aliyopiga Eden Hazard si ya kawaida kiasi hata Costa asingefunga,
bado tu Chelsea wangepata mabao kwa njia zingine.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...