Meneja Uhusiano wa Umma  wa Vodacom Tanzania, Matina Nkurlu (kulia) akiwakabidhi rasmi vijana wa kundi la”WAKALI SISI”la kiwalani jijini Dar es Salaam simu zao aina ya Vodafone Smart Kicka,ambazo ni moja kati ya zawadi walizojishindia  katika fainali za shindano la Dance 100% hivi karibuni na kujishindia kitita cha  Tsh Milioni 5 na simu hizo zimeunganishwa na mtandao wa Vodacom Tanzania  muda wa maongezi kiasi cha  shilingi laki moja.
 Mabingwa wa shindano la Dance 100% 2014” WAKALI SISI”wakimsikiliza  kwa makini Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(kulia) wakati alipokuwa akiwahusia kuhusiana na matumizi mazuri ya simu  baada ya kuwakabidhi rasmi ya simu zao aina ya Vodafone Smart Kicka zilizounganishwa na Vodacom na muda wa maongezi wa kiasi cha  shilingi laki moja ambazo ni moja ya zawadi walizojishindia katika fainali ya shindano hilo na kuibuka washindi wa kwanza na kujizolea kombe pamoja na kitita cha shilingi milioni 5.
 Kiongozi wa kundi la”WAKALI SISI” la Kiwalani jijini Dar es Salaam,Baraka Kambona(kushoto) akipokea mfuko wenye simu aina ya Vodafone Smart Kicka zilizounganishwa na mtandao huo na kuwekewa muda wa maogezi wa shilingi laki moja toka kwa Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu ikiwa ni kati ya zawadi walizojishindia katika fainali ya shindano la Dance 100% hivi karibuni na kuondoka na kitita cha  Tsh Milioni 5.
  Mabingwa wa Dance 100% 2014”WAKALI SISI”wa Kiwalani jijini Dar es Salaam,wakionesha simu aina ya Vodafone Smart Kicka  zikiwa na muda wa maongezi wa shilingi laki moja mara baada ya kukabidhiwa rasmi na Meneja Uhusiano wa Umma wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu (kulia)kundi hilo liliibuka mshindi wa kwanza  katika fainali ya shindano hilo hivi karibuni ambapo walijinyakulia kitita cha shilingi milioni 5.
Kundi la”WAKALI SISI”ambalo ni mabingwa wa shindano la Dance 100% 2014 wakionesha makali yao ya kucheza dansi katika makao makuu ya Vodacom walipofika katika hafla fupi yakukabidhiwa  rasmi ya simu zao aina ya Vodafone Smart Kicka zilizounganishwa  na muda wa maongezi wa kiasi cha shilingi laki moja ambazo ni moja ya zawadi walizojishindia katika fainali ya shindano hilo na kuibuka washindi wa kwanza na kujizolea kombe pamoja na kitita cha shilingi milioni5.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...