Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Iddi (wa pili kulia), akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dkt. Ramadhan Dau, alipotembelea mradi wa nyumba zinazojengwa na shirika hilo, Kijichi, Dar es Salaam leo. Kulia ni Meneja Miradi wa NSSF, Mhandisi John Msemo. 
Makamu wa pili Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi (kulia), Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dkt. Ramadhan Dau (kulia) na Meneja Miradi wa shirika hilo, Mhandisi John Msemo, wakimwangalia mke wa Makamu wa pili wa Rais, Mama Asha Seif, wakati akionyesha michoro wa nyumba ziliomvutia, walipotembelea mradi wa ujenzi wa nyumba za kisasa, Kijichi Dar es Salaam
Makamu wa pili Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi (wa pili kulia), akiwasikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Dkt. Ramadhan Dau (kulia kwake) na Meneja Miradi wa NSSF, Mhandisi John Msemo, wakati wakimuonyesha baadhi ya nyumba za kisasa zinazojengwa na shirika hilo, Kijichi, Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhhi ya Jamii (NSSF), Dkt. Ramadhan Dau (wa tatu kushoto), akimuonyesha Makamu wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Balozi Seif Iddi, baadhi ya nyumba zinazojengwa na shirika hilo, Kijichi, Dar es Salaam leo. Wa pili kulia ni Meneja Miradi wa NSSF, Mhandisi John Msemo.
 Mhandisi Msemo akitoa maelezo ya mradi kwa Makamu wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Iddi. Kulia ni Mkewe Mama Asha Iddi na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Dkt. Ramadhan Dau
Baadhi ya nyumba za kisasa zinazojengwa na NSSF Kijichi, Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...