Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa aliyekuwa Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Professa Rogath Kivasi, wakati alipofika kutoa pole nyumbani kwa marehemu Goigi jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2014.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimfariji mke wa ,marehemu Prof. Amelia Kivasi, wakati alipofika nyumbani kwa marehemu Goigi jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2014 kwa ajili ya kutoa pole msiba wa Prof. Rogath KIvasi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiagana na baadhi ya waombolezaji wakati akiondoka baada ya kutoa pole na kusaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa Professa Rogath Kivasi, Goigi jijini Dar es Salaam, leo Oktoba 7, 2014. Picha na OMR.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...