Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeo (CHADEMA) - Zanzibar,Bw. Salumu Mwalimu (kulia) akikabidhiwa vifaa vya ofisi kutoka kwa mtangulizi wake,Bw. Hamad Yusuf (kushoto) wakati wa hafla ya kumkaribisha iliyofanyika kwenye ofisi za chama hicho Daraja bovu mjini,Zanzibar jana.Katikati ni Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa.
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeo (CHADEMA) - Zanzibar,Bw. Salumu Mwalimu akiongea kwenye mkutano wa ndani baada ya kuwasili kwenye ofisi za chama hicho Daraja bovu mjini Zanzibar jana.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa akiongea na wanachama na viongozi wa Chadema jana
Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeo (CHADEMA) - Zanzibar,Bw. Salumu Mwalimu akipokewa na viongozi wa chama hicho baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Zanzibar akifuatana na Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk.Wilbrod Slaa (kulia) na viongozi wengine wa chama hicho jana.
Sehemu ya Wanachama na wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeo (CHADEMA) wakiwa kwenye mapokezi ya Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Salumu Mwalimu baada ya kuwasili kwenye ofisi hiyo Darajabovu mjini Zanzibar jana.
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa akiteta jambo na Manaibu wake,Mh. John Mnyika - Bara (kushoto) na Salumu Mwalimu - Zanzibar (kulia) kwenye mkutano na wanachama na viongozi wa chama hicho jana.
Wanachama na wapenzi wa Chadema wakimsikiliza Dk.Slaa alipozungumza nao kwenye ofisi za chama hicho huko Darajabovu mjini Zanzibar jana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Hapa CHADEMA naona kama wameliwa, maana hao ninaowaona na ambao ninawajua kwa yakini ni wapenzi/wanachama wa CUF ambao nadhani huenda ikawa wameazimwa ili kuwazuga akina Padri Slaa!!!! Tusubiri uchaguzi tuone.

    ReplyDelete
  2. Kwanza kabisa mi napenda demokrasia a nguvu zote ya kupigania demokrasia lakini CHADEMA hauka mwenye sura ya kuwa Rais kabisa hata mfanyeje! zHuyu slaa sioni kama ana confidence hata kidogo yaani kwa kumwangali tu mi nakosa hope! Tutafuteni mtu kama tunataka madaraka

    ReplyDelete
  3. Hongera Salumu piga kazi sasa kupanua demokrasia hapo zenji ili Chadema ichukue nafasi ya CCM/CUF. Voda watakuzingua muda sio mrefu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...