Afisa wa Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Bibi Ellen Maduhu akisoma hotuba katika Kamati ya Tatu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani.
Na. Ally Kondo, New York
Serikali imetahadharisha kuwa endapo mchakato wa kuandaa Agenda ya Maendeleo baada ya Mwaka 2015 unaoendelea hivi sasa katika Umoja wa Mataifa, hautazingatia mahitaji ya watu wenye ulemavu, dhamira ya kufikia maendeleo endelevu itakuwa ni ndoto kwa kuwa katika kila idadi ya watu watano duniani, mmoja wao ana ulemavu.
Kauli hiyo ilitolewa na Bibi Ellen Maduhu, Afisa wa Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, alipokuwa anahutubia wajumbe wa Kamati ya Tatu ya Umoja huo jijini New York, Marekani siku ya Jumatano tarehe 08 Oktoba 2014.
Bibi Maduhu alieleza kuwa wakati utekelezaji wa Malengo ya Milenia unafikia kikomo mwaka 2015, ni muhimu watu wenye ulemavu wakashirikishwa kikamilifu katika shughuli za maendeleo. Aidha, ni vema nchi zikawa na utaratibu mzuri kuhakikisha kuwa kundi la watu wenye ulemavu linafaidika na hatua za maendeleo zinazopigwa, kwa kuwa hiyo ni haki yao na ni wajibu wakapatiwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...