unnamed3Naibu waziri wa Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri akiwa na wataalamu na Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu wakikagua msitu wa Siha mkoani Kilimanjaoro alipotembelea juzi . Waziri Nyalandu aliruhusu nguzo nza umeme kupita katika msitu huo ili kuwezesha wananchi wa wilaya hiyo kupata umeme.
unnamedWaziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akimsalimia mmoja wa wagonjwa waliofuata huduma katika zahanati ya Ngarenanyuki wilayani Arumeru ,juzi  alipoitembelea baada ya Mbunge wa jimbo hilo kumlalamikia kuhusu tozo ya ushuru wa magari na wagionjwa wanaopita katik Hifadhi ya Taifa ta Arusha ili kupata huduma katika hospitali hiyo. Waziri Nyalandu aliamuru wananchi wanaohitaji kupata tiba katika zahanati hiyo kupita bure hifadhini. unnamed1Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari akimtaarifu Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu juu ya adha wanayopata wananchi wa jimbo klake wakati wakiiingia katika Zahanati ya tiba za Asili cha Ngarenanyuki mkoani Arusha juzi , kutokana  na tozo la pesa kupitia hifadhi ya Taifa ya Arusha. Waziri Nyalandu aliamuru wananchi wanaohitaji kupata tiba katika zahanati hiyo kupita bure hifadhini. unnamed2Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akiwa na Mbunge wa Siha ambaye ni Naibu waziri wa Serikali za Mitaa, Aggrey Mwanri wakikagua kitalu cha miti katika shamba la mitiulioko wilayani humo juzi. Waziri Nyalandu aliruhusu nguzo nza umeme kupita katika msitu huo ili kuwezesha wananchi wa wilaya hiyo kupata umeme n akuondoa mgogoro uliozuia mradi huo kwa muda mrefu.
……………………………………………………………..
Serikali imepiga marufuku ukataji wa miti nchini hata kama ikiwa mtu amepanda nyumbani kwake anatakiwa kuomba kibali kwajili ya kukata mti huo.

Akizungumza wilayani Siha juzi ,Waziri wa Maliasili na Utalii , Lazaro Nyalandu amesema kwamba Tanzania inawez a kuwa jangwa baada ya miaka 15 kutokana na uvunaji mbaya wa bidhaa za miti unaofanyika nchini .
“Tukiendelea kukata miti kma hivi tutakuwa tunatengeneza janga la kitaifa kwa hiyo kwa sasa naomba niseme rasmi kuwa hakuna mtu anaruhusiwa kukata miti au mti hata kama ameupanda nyumbani kwake, ni lazima aombe kibali kwa maafisa wa misitu. Tunatakiwa kushiriki kwa pamoja katika kutunza mazingira yetu” alisema.

Nyalandu alisema kasi ya ukataji miti nchini imekuwa kuubwa kwa sasa kutokana na kuongezeka kw aidadi ya watu na kuwa kwa mwaka mmoja pekee hekta 350,000 hukatwa huku kikiwa hakuna jitihada za kurejesha iliyoondolewa.

“Kwa kaddri siku zinavyozidi kwenda na watu kuongezeka baada ya miaka kumi misitu itakuwa inavunwa kw azaidi ya hekta 850,000 nchini kwa mwaka, hii ni hatari kubwa, lazima tufanye jitihada zaidi kukomesha tatizo hili”.

Aliwaagiza wakuu wa wilaya za Arusha na kilimanjaro kuunda timu ili kuandaa  hadidu za rejea kwa ajili ya kupatia kikosi kazi ambacho kitaandaas andiko kw ajili ya kuanzisha mfuko huo.

Mtendaji Mkuu wa wakala wa misditu (TFS) Juma Mgoo alisema kwamba misitu ilianza kutunzwa mtokea enzi za wakoloni lakini tatizio kubwa linalotokea kw asasa ni watu wengi kuivamia kutokana na mahitaji ya nishati na uchomaji wa misitu.

Alisema kwamba kwa msitu wa asili kawaida huwa na mita 30 za ujazo wakati kwa upande wa misitu ya kuoandwea huwa wna ujazo wa zaidi ya mira za ujazo 400 hadi 600 kitu ambacho alishauri  umuhimu w akupanda miti zaidi ili iweze kukabiliana na ongezeko la mahitaji na kuokoa misitu iliyopo.

Waziri Nyalandu alitoa maagizo ya kuruhusu nguzio za umeme kupita katika msitu wa wilayani Siha ili kufanywa wananchi waweze kupata nishati ya umeme ili kuokoa matumizi ya kuni kama nishati na kulinda misitu.

“Umemem ni nishati mbadala badala ya kuni na mkaa kwa hiyo napenda kuwaeleza kwamba ni bora miti michache ikatwe ili pupisha nguzi za umeme ili wananchi wakipata nishati hiyo waache kutumia kuni na kuharibu misitu na kutumia umeme kama nishati mbadala” alisema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. UKWELI NI KWAMBA HAPO WAZIRI NYALANDU AMEC HEMSHA HUO NI UTAWALA WA KIDIKTETA, HUWEZI KUMZUWIA MTU KUKATA MTI WAKE WAKATI YEYE ALIUPANDA KWA MALENGO YAKE, UKWELI NI KWAMBA WENGI WETU ATATUFUNGA NA SHERIA IPO TUTABURUZANA MAHAKAMANI. BADALA YAKE ANGEWEKA MAZINGIRA YA KUHIMIZA WANANCHI WAKE KUPANDA MITI NA SIO KUKATA MISITU YA ASILI, MITI NIMEPANDA KWA MALENGO YANGU UKIFIKA MDA NITAKATA NIONE ATAKAE NIZUWIA, INATAKIWA IFIKE WAKATI VIONGOZI WENYE AMRI ZA KIDIKTETA WANG'ATUKE.

    ReplyDelete
  2. BIG UP NYALANDU! UMEFANYA BUSARA SANA NA UMEONESHA UZALENDO KWA NCHI YAKO. SHERIA HII ITASAIDIA SANA KUWEKA MAZINGIRA YETU KATIKA HALI YA USAFI. AIDHA SHERIA HII SIO NGENI KWANI IMESAIDIA NCHI NYINGI SANA KUBORESHA MAZINGIRA MFANO HUKU CHINA. MTU HARUHUSIWI KUKATA MTI NA WANACHOFANYA KUNA IDARA MAALUMU YA MISITU NDIO WANAHUSIKA UKATAJI MITI. JAMAA WANAHESHIMU SANA MITI. NAIKITOKEA KUWA MTI INABIDI UONDOLEWE BASI MTI HUO HUONDOLEWA NA KUOTESHWA SEHEMU NYINGINE. INABIDI TUFIKE MAHALA TUWAIGE RWANDA KWA UTUNZAJI MAZINGIRA NA KUWEKA NCHI SAFI. BIG UP NYALANDU IKIWEZEKANA WEKA SHERIA YA USAFI WA LAZIMA KILA MWISHO WA JUMA.

    ReplyDelete
  3. Amri hizi zinazotolewa kwa kukurupuka zinasababisha viongozi ngazi za chini kuzitumia kunyayasa wananchi. Kiongozi inabidi upime madhara ya amri kabla ya kuitoa!!

    ReplyDelete
  4. Kweli kabisa mdau hapi juu. Waziri amechemka haswaa. Mti niupande mwenyewe kwa starehe zangu, niugharamie na kuuangaikia muda siutaki natakiwa niombe jibali...??? Huo ni uonevu. Km serekali mnatakiwa muwe na mikakati ya kuendeleza na kuboresha misitu na si kuwapa amri wananchi kwenye makazi yao. Tanzania tuna maeneo mengi yanayoweza kupandwa miti ila hakuna mikakati wala malengo mnaishia kunyanyasa na kuwabana raia.

    ReplyDelete


  5. hahahahaaaaaa Nyalandu umenichekeshaaaa!!!
    hahaaahaaaaaa! u r not serious!! r u?hahaaaaaa!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...