Pichani
juu na chini ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na
mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini,
Alvaro Rodriguez akimtambulisha mgeni rasmi Waziri wa Ardhi , Nyumba na
maendeleo ya makazi Profesa Anna Tibaijuka kwa baadhi ya wakuu wa
mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini mara baada ya kuwasili kwenye
sherehe za maadhimisho ya miaka 69 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa
kwake.

Waziri
wa Ardhi , Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka
akipokea heshima ya wimbo wa taifa kabla ya kuanza rasmi kwa sherehe za
maadhimisho miaka 69 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake.
Waziri
wa Ardhi , Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka
akikagua gwaride maalum kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 69 ya
Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake zilizofanyika leo jijini Dar.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...