Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limepokea mwili wa Marehemu Meja Jenerali Muhidini Mfaume Kimario (Mstaafu) kutoka nchini India leo tarehe  09 Oktoba, 2014 katika uwanja wa Kimataifa wa Mwl JK Nyerere Dar es salaam,mwili wa marehemu umewasili kwa Shirika la ndege la Ethiopia saa 7:30 mchana.  

Mwili wa marehemu utaagwa kesho tarehe 10 Oktoba, 2014 saa 4:00 asubuhi katika viwanja vya hospitali Kuu ya Jeshi Lugalo na baadaye mwili utasafirishwa kwenda kwao Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro kwa mazishi yatakayofanyika tarehe 11 Oktoba, 2014 saa 7:00 mchana siku ya Jumamosi.              

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mh.  Dkt Hussein Mwinyi anatarajiwa kuongoza waombolezaji kutoa heshima za mwisho.

MUNGU AILAZE MAHALI PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU
MEJA JENERALI MUHIDINI KIMARIO (MSTAAFU)
AMINA

Imetolewa  na:

Kurugenzi  ya  Habari  na  Mahusiano
Makao Makuu ya Jeshi, 
Upanga

S.L.P  9203,   
Dar es Salaam,  
Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mwanafunzi wakoOctober 10, 2014

    Inna Lillah wa inna Ilayh rajiuun Mola akuweke pema peponi Mwalimu wetu Ameen!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...