Menejimenti ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) inasikitika kutangaza kifo cha mfanyakazi mwenzao Bw. Amin Elias Mbaga aliyekuwa Meneja Uhusiano kilichotokea tarehe 13.10.2014 katika Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam. Mipango ya Mazishi inafanyika nyumbani kwa marehemu Sinza Kumekucha.

Ibada ya kumuombea marehemu itafanyika tarehe 15/10/2014 katika Kanisa la KKKT Sinza Kumekucha kuanzia saa saba mchana na baada ya ibada safari ya kusafirisha mwili wa marehemu kwenda Same kwa maziko itaanza.

Maziko yanatarajia kufanyika katika kijiji cha Muhezi Mwembe Mlimali Same siku ya Alhamisi tarehe 16/10/2014.

 Amin tulikupenda lakini Mungu amekupenda zaidi pumzika kwa Amani. 

Amen.

Imetolewa na menejimenti ya Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Rest in peace my mate,nisalimie Mzobora.
    v mashamba

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...