Mchakato wa uuzaji na ununuaji wa bidhaa umerahisishwa sana kwa kadri waendashaji wa makampuni ya biashara kwa njia ya intaneti wanavyozidi kuwa wabunifu na wagunduzi zaidi.
Kaymu Tanzania, kampuni inayoongoza kwa kuuza na kununua vitu kwa njia ya mtandao imejitanua zaidi baada ya kuzindua app (programu ya simu) yake Septemba 2014.
Kaymu Tanzania imezindua huduma zake za kwanza za programu ya simu nchini, hivyo kuwawezesha watumiaji wa Android kufanya manunuzi ya bidhaa na kuweka oda moja kwa moja kupitia simu zao za viganjani, na kuwawezesha pia wauzaji kusimamia maduka na oda zao kwa uharaka na uwepesi zaidi.
Akizungumza na wanahabari kwenye makao makuu ya kampuni hiyo hapo Mikocheni- Dar-es-salaam, Mkurugenzi mtendaji wa Kaymu Tanzania Erfaan Mojgani alisema, “Programu hii ina matumizi yote yanayotakikana, kuwawezesha wanunuaji kutimiza muamala wowote ikiwemo: kutembelea maduka na kuangalia aina tofauti za bidhaa mbali mbali, kuweka oda, na hata kuwasiliana moja kwa moja na wauzaji katika mchakato huo"
Kwa kuongezea, application (programu) hii – inayopatikana kwenye Google Play Store – haina makato yoyote ya pesa kwa watumiaji wa "smartphone" wanaotumia mtandao wa Tigo. Mnunuaji au muuzaji yoyote anaweza akadownload hii application, na akafungua akaunti yake na kuitumia kwa kupitia intaneti.
“Faida za programu hii ni kubwa pia kwa wauzaji, ikiwarahisisha uwekaji wa picha za bidhaa mpya na ikiwapa wepesi wa kusimamia accounts zao, kuhariri orodha ya bidhaa, na kuona mauzo yao” Erfaan aliongezea.

Kwa kutambua kuwa asilimia kubwa ya ongezeko la watumiaji wa intaneti nchini Tanzania wanatumia intaneti kupitia simu za mikononi, Kaymu imedhihirisha jinsi ilivyojikita kwenye suala la ubunifu na kuwapa wateja wao uwezo wa kutumia hii app (programu) kwa urahisi zaidi. Zaidi ya hayo, kuonyesha kuwa watumiaji wa iphone hawajasahaulika, Erfaan aliongezea kuwa application hii kwa watumiaji hao tayari iko katika matengenezo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Jamani Hawa jamaa ni magumashi tu . They dont deliver whatever you buy

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...