Kampuni maarufu ya kuuza muziki kwa njia ya digitali inayojulikana kama Deezer, imeingia ushirikiano na kampuni ya Vodacom ambapo wateja wa Vodacom wataweza kupakua muziki katika maktaba kubwa ya muziki ya kampuni hiyo yenye nyimbo zaidi ya milioni 35.
Deezer ni kampuni kubwa ya kuuza muziki kwa njia ya kidigitali nchini Afrika ya kusini.Katika kusherehekea ushirikiano huu na Vodacom wateja wapatao 17 milioni wa Vodacom watajipatia offer ya kipindi cha mwezi mmoja ya kupakua bure muziki wa aina mbalimbali kutoka maktaba kubwa ya muziki ya kampuni ya Deezer.
“Kupitia ushirikiano huu wateja na wapenzi wamuziki nchini Afrika ya Kusini wataweza kupata muziki kutoka sehemu mbalimbali duniani na uzuri wa huduma hii ya kiteknolojia ni rahisi kinachotakiwa ni kujisajili na kuanza kupakua muziki uupendao kutoka maktaba kubwa ya muziki wa kidijitali ya Deezer”Anasema Phil Patel,Mtendaji Mkuu wa Uendelezaji wa Biashara wa Vodacom.
Kufaidi huduma hii anachopaswa kufanya mteja wa Vodacom popote alipo ni kujisajili kwa kutembelea tovuti ya http://live.vodafone.com/deezer.Baada ya kujisajili itakuwa rahisi kuanza kupakua muziki aupendao,offer ya mwezi mmoja ya kupakua muziki bure imeanza oktoba 9 mwaka huu.
BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI
BOFYA HAPA KWA HABARI KAMILI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...