Waziri
Mkuu, Mizengo Peter Pinda amewataka Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuendana
na kasi ya Mpango wa MATOKEO Makubwa Sasa (BRN) katika utendaji wao hasa
katika eneo la ufuatiliaji na uadilifu.
Waziri
Mkuu Pinda ameyasema hayo leo (Jumatano) mjini hapa wakati wa hotuba
yake fupi ya ufunguzi wa Mkutano wa siku tatu wa watendaji hao
kujitathmini katika utekelezaji wa miradi ikiwemo miradi ya elimu
iliyoko chini ya BRN. Mkutano huo umeandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu –
TAMISEMI.
BRN
ni Mpango ulioasisiwa na Serikali ya Tanzania na kuanza kazi Julai
mosi, 2013 ukiwa na malengo ya kuleta mfumo mpya wa kuweka vipaumbele,
kutekeleza miradi kwa wakati na watendaji kuacha kufanyakazi kwa mazoea.
Sekta
sita za awali zilizoingizwa katika vipaumbele vya BRN ni elimu, maji,
kilimo, nishati, uchukuzi na ukusanyaji wa mapato. Sekta za uboreshaji
wa mazingira ya biashara na afya ziko mbioni kuingia katika BRN.
Utekelezaji wa BRN unasimamiwa na Kitengo kipya cha Rais cha Usimamizi
wa Miradi (PDB).
Bw.
Pinda alitumia muda huo kusisitizia kuwa BRN imeleta kasi nzuri katika
utekelezaji wa miradi kwa kusisitizia uwajibikaji na malengo.
Aliwahamaisha viongozi hao kushirikiana na wataalamu mbali mbali
wanaofanya kazi zao katika maeneo ya mikoa na wilaya ili kufanikisha
maendeleo ya Taifa.
Akifafanua
zaidi utendaji kazi chini ya BRN, Waziri Mkuu alisema Mpango huo
unawalazimu watendaji hao kuwajibika ipasavyo katika ushirikishaji,
usimamizi makini na ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi mbali mbali ya
Serikari.
Alitumia
pia fursa hiyo kuwataka viongozi hao waandamizi kuhakikisha kuwa katika
utekeleaji huo wa miradi unakuwepo ushirikiano na wakandarasi wenye
sifa kwani ubadhirifu na upendeleo katika utoaji wa miradi umekuwa
ukirudisha nyuma maendeleo na kuwakwaza wananchi.
Kwa
upande wake Mratibu wa Masuala ya Utawala Serikalini kutoka Ikulu,
Francis Mang’ila siri ya nchi kupata maendeleo ni kwa watendaji wote
ngazi za mikoa na wilaya, kutatua malalamiko mbali mbali yanayowafikia
kwa kuzingatia wakati badala ya kuacha wananchi wakilalamika.
Alisema
hali iliyopo sasa inapaswa kubadilika ambapo badala ya wananchi
kuwasilisha zaidi matarajio wamekuwa wakiwasilisha malalamiko kutokana
na watendaji waandamizi wa mikoa na wilaya kushindwa kufanyiakazi kero
zao mapema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...