Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira, Dkt. Binillith S.Mahenge akipewa maelezo na Mratibu wa NEMC kanda ya Ziwa Bi. Anna Masasi kuhusu uharibifu wa Mazingira ya Mwambao wa Ziwa Viktoria katika eneo la Nera, unaosababishwa na shughuli za Kilimo na ufugaji wa samaki katika eneo hilo jijini Mwanza.
Sehemu ya mwambao wa Ziwa Viktoria katika eneo la Nera jijini Mwanza likionesha shughuli za kilimo zinazofanyika katika eneo hilo na kusababisha uharibifu wa mazingira akioneshwa jinsi taka za plastiki zinavyochakatwa kutwnwza bi ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa magugu maji kunakosababishwa na mbolea inayotumika katika shughuli za kilimo.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira, Dkt. Binillith S.Mahenge akioneshwa jinsi taka za plastiki zinavyochakatwa kutengeneza bidhaa mbalimbali, kama vile Mifuko ya Plastiki, alipotembelea kiwanda cha Falcon Parkaging Ltd cha jijini Mwanza. Anayetoa maelezo ni Mkurugenzi wa Kiwanda Bwana Ganeshan Vedagiri.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira, Dkt. Binillith S.Mahenge akioneshwa mbao iliyengezwa kutokana na taka za plastiki katika kiwanda cha Falcon Packaging Ltd cha jijini Mwanza.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira, Dkt. Binillith S.Mahenge akioneshwa mifuko ya plastiki inayotengenezwa na kiwanda cha Falcon Packaging Ltd kutokana na taka za plastiki zinazokusanywa katika maeneo mbalimbali ya jiji la Mwanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. This Minister is such a great man, msikilizeni anavyowaelekeza, hana ubaya wala hiyana na mtu bali ni mpenda nchi yake tu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...