Wajumbe wa Kamati Tendaji ya BAMMATA katika picha ya pamoja mara baada ya kikao cha Kamati hiyo kilichofanyika jijini Mbeya katika Bwalo la Magereza la Chuo Ruanda.Wa tatu kutoka kushoto mstari wa mbele ni mwenyekiti wa Baraza hilo Brigedia Jenerali CIRIL MHAIKI.
Tanzania imekuwa haifanyi vizuri sana katika michezo mingi ya Kimataifa inayoshiriki kwa hivi sasa.Hii inatokana na changamoto nyingi zinanazoikabili Taifa miongoni mwake ikiwa ni kutokuwapo kwa michezo ya majeshi kama ilivyokuwa hapo awali.
Michezo hiyo ambayo ilikuwa inasimamiwa na Baraza la michezo ya Majeshi Tanzania (BAMMATA) ilikuwa inatumika kubaini na kuendeleza vipaji vya wanamichezo wanajeshi ambao walitumika kuitangaza Tanzania kimichezo nje ya nchi na hivyo kuliletea heshima na sifa maridhawa Taifa letu.
Baadhi ya wachezaji walioliletea taifa sifa kwa uchache ni pamoja na Filbert Bay, Juma Ikangaa, Samson Ramadhan, Iswege Christopher,Nasser Mafuru, Samuel Mwang’a , Hitii Shamba na Restuta Joseph ambao wote ama wametokea Majeshini au wamepata mafunzo na wakufunzi wa majeshini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...