Taarifa zilizotufikia hivi punde ndani ya chumba cha habari cha Globu ya Jamii,kinaleleza kuwa kaimu Mkurugenzi wa TPDC,Bwa.James Andilile na Mwenyekiti wake wa bodi Bwa.Michael Mwanda wamepelekwa rumande kwa kosa la kutowasilisha mikataba 26 kwa kamati ya bunge la  hesabu za mashirika ya umma PAC,kamati imeagiza wapelekwe huko na hatua zichukuliwe dhidi yao.

Kikosi kazi cha Globu ya Jamii kipo kazini kuifuatilia taarifa hii,hivyo tuendelea kupitia pitia hapa jamvini kupata Updates. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 5 mpaka sasa

  1. Hivi kamati ya Bunge inaweza kumuamuru mtumishi wa umma awekwe rumande kwa kushindwa kufanya jambo fulani na hiyo amri ikatekezwa? Na ni sheria ipi inairuhusi hiyo kamati kufanya hivyo. Naomba ufafanuzi wadau mimi hapo sielewi!

    ReplyDelete
  2. kama sijakosea hakuna sheria inayozuia hiyo mikataba isiende bungeni; sasa mpka kuwekwa rumande tatizo lipo wapi kwa mtumishi wa wananchi?ni jambo la ajabu! MALI ZOTE ZILIZOKO KWENYE ARDHI HII NI ZETU SISI TUNAOISHI KATIKA ARDHI HII.

    ReplyDelete
  3. Du! Tuone itaishia wap? Kama wezi wa EPA walisaamehewa kwa wizi wao, hawa itaishia juu kwa juu.

    ReplyDelete
  4. Sasa wanaficha ,nini? Kama taratibu zote zimefuatwa? Hiyo mikataba Ni kwa faida ya nani? Kama Ni kwa faida ya watanzania, basi wawakilishi WA wananchi wapewe nafasi ya kuiona.

    ReplyDelete
  5. Mnaogombea kupewa Uongozi mmeona makali yake?

    Zama hizi ni bora nichukue Jembe nikalime kuliko kukubali kubeba madaraka ni sawa na kujitwisha mgongoni gunia la misumari!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...