Na Andrew Chale

ASIA Idarous Khamsin na Safari  Carnival  wanakuletea usiku wa Khanga Party na Spice Modern Taarab watakaowasha moto wa burudani sambamba na gwiji wa mipasho nchini Khadija Kopa pamoja na Bilal Mashauzi,  Jumamosi ya usiku wa Novemba 29, ndan ya ukumbi wa Safari Carnival, Mikocheni B.

Kwa mujibu wa  mmoja wa wandaaji wa usiku huo, Asia Idarous Khamsin,  amesema tayari maandalizi yake yamekamilika na amewasihi wadau kujitokeza kwa wingi katika onesho hilo la aina yake  kwa kiingilio cha sh 10,000 na 20,000 kwa V.I.P.

Asia Idarous Khamsin alisema Usiku wa Khanga, itaanza kuanzia usiku wa saa mbili  na kuendelea huku vazi maalum likiwa ni Khanga.

"Usiku huu ni maalum kulienzi vazi la khanga, ambalo pia ndilo vazi maalum la usiku huo. Pia watafurahia muziki mzuri kutoka kwa magwiji wa taarab hapa nchini akiwemo Khadija Kopa, Spice Modern taaba na Bilal Mashauzi." alisema Asia Idarous Khamisin  ambapo pia alisisitiza vazi la khanga ni la heshima hasa kwa mwanamke wa Kitanzania hivyo kila mmoja atakapolitengeneza vizuri ama kufunga litamweka malidadi.

Aidha, alibainisha kuwa, usiku huo pia kutakuwa na  zulia jekundu 'Red Carpet' ambapo watu mbalimbali watapata kupiga picha na mastaa na watu maalufu watakao jitokeza usiku huo.

Pia alibainisha kuwa, tayari tiketi zimeanza kuuzwa sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam ikiwemo Fabak fashions Mikocheni na Safari Carnival  kwa mawasiliano piga 0754263363 au 0713263363

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...