Walimu  (ma-Sensei) watano toka Tanzania, yaani Sensei Dudley Mawalla, Sensei Daud Magoma, Sensei Kheri Kivuli, Sensei Edgar Kaliboti na Sensei Rumadha Fundi, wanatoa shukrani  nyingi sana kwa  kupewa dhamana kubwa ya heshima na vyeo vya ngazi za juu toka shirikisho la Karate Tanzania (Tanzania Karate-Do Federation). 
 Chini ya uongozi wa mwenyekiti Sensei Geofrey Kalonga na katibu mkuu wake Sensei Phillip Chikoko, wana-sema ma-Sensei hao katika waraka ulioandikwa na Sensei Rumadha Fundi kwa niaba ya wote kuwa wao hawana  budi kuitikia wito wa kuchangia maendeleo ya sanaa ya Karate inayohitaji nidhamu na mifano ya ujasiri wa hali ya juu kwenye kizazi kipya cha taifa letu. 
 Sensei Dudley Mawalla na Sensei Daudi Magoma, walitunukiwa shahada au Dan ya Saba kila mmoja, wakati  Sensei Kheri Kivuli, Sensei Kaliboti na Sensei Rumadha Dan sita kila mmoja.
Sensei Dudley Mawalla, mwanzilishi wa Japan Shotokan Tanzania. Sensei Kaliboti, mkufunzi wa Gracie Ju jitsu, Australia, Sensei Rumadha, Okinawan Goju Ryu Jundokan KyoKai, Texas, USA, Sensei Daudi na Sensei Kivuli, wakufunzi wa Okinawa Goju Ryu, Dar Es Salaam, Tanzania.
 Sherehe hizo zilifanyika uwanja wa ndani wa taifa kuadhimisha siku ya baba wa taifa Mwalimu Nyerere, kushirikishwa na zaidi ya wana-Karate 50 wa ngazi mbalimbali toka shule na mikoa tofauti hapa nchini. 
"Wote tuliotunukiwa heshima hiyo, hatunabudi kusema asante zetu katika shirikisho la Karate Tanzania(Tanzania Karate-Do Federation", unamalizia waraka huo ambao Globu ya Jamii ina nakala yake
Katibu Mkuu wa Tanzania Karate Do Association Sensei Philip Chikoko (kushoto) akimtunuku  Sensei daudi Magoma shahada au Dan ya Saba

Katibu Mkuu wa Tanzania Karate Do Association Sensei Philip Chikoko (kulia) akimtunuku  Sensei Kheri Kivuli  shahada au Dan ya Sita
Sensei Edgar Kaliboti akiwa anasimamia mafunzo ya mtindo wa Gracie Ju jitsu huko Australia. Tanzania Karate do federation imemtunuku Dan ya sita
Sensei Dudley Mawalla akitunukiwa Dan ya saba na Mwenyekiti wa Tanzania Karate do Federation Sensei Godfrey Kalonga (kulia). Kushoto ni Katibu Mkuu wa Tanzania Karate Do Association Sensei Philip Chikoko
Sensei Rumadha Fundi akicheza kata. Yeye ametunukiwa Dan ya Sita

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...