Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Bwana Kyle Peters amefanya ziara katika kijiji cha Buma wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani ambako ameshuhudia walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na TASAF na kuridhishwa kwake na namna mpango huo ulivyowanufaisha walengwa ambao wameanza kuondokana na umaskini.

Akiwa kijijini hapo Bwana Peters alitembelea moja ya nyumba iliyoboreshwa na mmoja wa walengwa wa Mpango wa Kunusuru kaya maskini Bwana Bakari Rajabu Bakari ambaye kwa kutumia fedha za ruzuku kupitia Mpango wa kunusuru kaya maskini ameweza kuboresha maisha yake ikiwa ni pamoja na kununua Luninga(TV) huku akimudu pia kusomesha watoto wake.

Bwana Peters amesema utekelezaji wa Mpango huo umeanza kuonyesha mafanikio nchini TANZANIA  jambo ambalo litatumiwa na Benki ya Dunia kuendelea kuufadhili huku mfano huo ukisambazwa katika nchi nyingine ili kazi ya kuutokomeza umaskini iwe na mafanikio.

Akizungumza katika ziara hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga amesema mafanikio ya utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya maskini yanatokana na taasisi yake kuamini na kutekeleza majukumu yake kwa uwazi na kuwashirikisha wadau mbalimbali wakiwemo walengwa katika hatua za utekelezaji wake.

Zifuatazo hapo chini ni baadhi ya picha za ziara ya makau huyo wa Rais wa Benki ya Dunia katika kijiji cha Buma wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.
    Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kyle Peters akiwahutubia wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini katika kijiji cha Buma wilayani Bagamoyo.
    Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Ladislaus Mwamanga (aliyesimama) akitoa ufafanuzi wa masuala ya mpango wa kunusuru kaya masikini kwa walengwa (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kyle Peters.
0Baadhi ya wanuafaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini unaotekelezwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii – TASAF katika kijiji cha Buma wilyani Bagamoyo wakiwa katika picha ya pamoja na Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kyle Peters na Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Ladislaus Mwamanga.

    Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Ahmed Kipozi akimkaribisha Makamu wa Rais wa Benki ya Dunia Kyle Peters alipotembelea miradi ya TASAF wilayani humo. Kushoto kwake Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Ladislaus Mwamanga.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...