Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akiwaonyesha waandishi wa habari (hawapo pichani), moja kati ya mashine 4 za  kurudufu CD  feki zilizokamatwa katika eneo la Kimara jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Ofisa wa Polisi, D/SSGT Daniel Gingo. (Picha na Francis Dande)
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani), wino unaotumika kunakshia makasha ya CD feki wanazozitengeneza
Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotions, Alex Msama akiwaonesha waandishi wa habari (hawapo pichani), baadhi ya CD feki zilizokamatwa

=========  =======  =======  =======
KAMPUNI ya Udalali ya Msama Auction Mart ya jijini Dar es Salaam chini ya Mkurugenzi wake Alex Msama ikishirikiana na Jeshi la Polisi Kituo cha Urafiki na Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, imekamata kompyuta za kufyatua kazi feki za wasanii zenye thamani ya mil18.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Auction Mart, Alex Msama, alisema mitambo hiyo imekamatwa kwa ushirikiano mkubwa kati ya pande hizo tatu pamoja na sapoti ya wasamaria wema. Alisema kopyuta, mashine na kazi feki zenye thamani ya mamilioni ya fedha, zimekamatwa eneo la Kimara-Machungwani, jijini Dar es Salaam na mtuhumiwa huyo amefikishwa katika kituo cha Polisi kwa ajili ya mchakato wa kiheria wa kufikishwa mahakamani. 

Msama alisema akiwa mdau wa masuala ya burudani kupitia kampuni yake ya Msama Promotions Ltd ambayo imekuwa ikiratibu matamasha ya Muziki wa Injili, amekuwa akiguswa na kitendo wanjanja wachache kunufaika na jasho la kazi ya wengine.Alisema wizi wa kazi za wasanii mbalimbali umekuwa kikwazo cha mafanikio ya wahusika ambao licha ya kuifanya kazi hiyo kwa muda mrefu, wameshindwa kupiga hatua kiuchumi kutokana na wajanja hao kuingiza kazi feki mtaani ambazo huuzwa kwa bei ya kutupa.

Msama alisema kazi hiyo ngumu ambayo imekuwa ikifanywa na kampuni yake kwa kushirikiana na wadau wengine, anashukuru kwamba kadiri siku zinavyosogea wengi wamezidi kukamatwa kutokana na ushirikiano ambao wamekuwa wakipewa.“Msama Auction Mart tunachukua nafasi hii kulipongeza Jeshi la Polisi hasa Kituo cha Ubungo ambacho wamekuwa msaada mkubwa kwetu katika vita hii ya kupambana na
wezi wa kazi za wasanii,” alisema Msama.

Aliongeza, kwa ushirikiano mkubwa wa Jeshi la Polisi na Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, anashukuru kazi hiyo imekuwa ikisonga mbele kwa kazi feki kuzidi kukamatwa katika maeneo mbalimbali ya nchi katika kulinda maslahi ya wasanii.Alisema tangu kuanza kwa kazi hiyo ngumu ya kukabiliana na wizi wa kazi za wasanii, kampuni yake imekamata vifaa mbalimbali vya kukamilisha kazi hiyo na kazi zenye jumla
ya shilingi bil.12.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kama kweli serikali inataka kuwasaidia wasanii wangeanzisha itaratibu wa hatimiliki na kila msanii asajiliwe na basata. Radioni, tv, kuhojiwa, wawe wanalipwa kama wanavyofanya nchi zingine.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...