Mwanamuziki
Mkongwe kutoka bendi ya muziki wa dansi ya Twanga Pepeta Khamis T. Kayumbu, maarufu kama Amigolas (pichani kulia
enzi za uhai wake) amefariki
Dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili
jijini Dar es salaam.
Taarifa za awali ambazo chumba cha habari cha Globu ya Jamii imezipata kutoka kwa vyanzo vya kuaminika zinaeleza kuwa marehemu Amigolas alikuwa
akisumbuliwa na maradhi ya Moyo mpaka kufariki kwake.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Twanga Pepeta, msiba uko nyumbani kwa mama wa marehemu Mburahati, jirani na shule ya Msingi ya Mianzini.
Mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho Jumatatu alasiri katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi kutoka Twanga Pepeta, msiba uko nyumbani kwa mama wa marehemu Mburahati, jirani na shule ya Msingi ya Mianzini.
Mazishi yanatarajiwa kufanyika kesho Jumatatu alasiri katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam.
Amigolas atakumbukwa kwa sauti yake nzuri na utanashati awapo jukwaani. Wimbo "Aminata" alioutunga na kuuimba akishirikiana na Ally Choki, Msafiri Diof, Lwiza Mbuttu na Jessica Charles ni moja ya nyimbo bora za Twanga Pepeta wakati huo hadi sasa. Usikilize hapo chini.
Mungu ailaze roho ya Marehemu mahali pema peponi
-Amin
-Amin
Taifa limepoteza nguli wa mziki
ReplyDeleteRest In Peace My Friend Amigolas.
ReplyDeleteP.Owino
RIP Amigolas!
ReplyDelete724
Inna lillah wainnailah Rajiun
ReplyDeleteWadau
Ngoma Africa Band (FFU)