Marehemu
Eng. John Said Kimbe
Jumuiya ya Watanzania Mozambique (JUWAMO) inasikitika kutangaza kifo
cha Ndugu yao Mpendwa Eng. John Said
Kimbe, kilichotokea ghafla usiku wa tarehe 10 Novemba, 2014 nyumbani kwake
Maputo, Mozambique.
Wakati wa uhai wake, marehemu alikuwa Mwenyekiti wa JUWAMO,
Tawi la CCM Maputo, Mozambique na Mfanyakazi; Mtaalamu wa Miundombinu ya
Mawasiliano “Telecommunication/ICTs expert” kwenye Jumuiya ya Maendeleo Kusini
mwa Africa (SADC), kitengo cha “Southern Africa Telecommunications Association (SATA) tangu Juni 2001.
Jumuiya ya
Watanzania Mozambique inawafahamisha Watanzania wote waishio Jiji la Maputo na
vitongoji vyake kuwa mwili wa marehemu unatarajiwa kuagwa “Memorial Service”
tarehe 13 Novemba, 2014 katika Kanisa la Roman Catholic “Paroquia Nossa Senhora
das Victoria” Karibu na Soko la Janet – Maputo, saa 9. Mwili wa marehemu
unatarajiwa kusafirishwa kwenda Tanzania kwa mazishi tarehe 14 Novemba, 2014.
JUWAMO
inawaomba Watanzania wote kujitokeza kumuaga mpendwa wetu na kuwafariji wafiwa
kama mila na desturi zetu zinavyotuelekeza.
Kwa
mawasiliano zaidi wasiliana na Katibu wa JUWAMO Ndugu Annuar Aziz Simu No.
+258824034391 au +258842337117 na Katibu wa CCM –Tawi la Maputo, Mozambique
Ndugu Gesona Ngabo Simu No. +258821403433.
Imetolewa na JUWAMO
12/11/2014
Mwenyezi Mungu ailaze pema roha ya marehemu Kimbe Amen...
ReplyDeleteInnalillah wa innalilahi rajiuuna. Kila nafsi itaonja mauti.
ReplyDeleteRIP Dady
ReplyDeleteIsaelly