Na John Gagarini, Bagamoyo

SUALA la Maabara kwa shule za Sekondari za Kata limeingia kwenye hatua nzito baada ya mkuu wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza kuiacha ofisi yake na kuhamia Wilaya ya Bagamoyo ili kuhakikisha agizo la Rais Dk Jakaya Kikwete la kila wilaya iwe imekamilisha ujenzi huo ifikapo Novemba 30 mwaka huu.

Sambamba na hilo mkuu huyo amewataka wakuu wa idara wa Wilaya hiyo kila mmoja kutokaa ofisini na kuchagua kata ya kwenda ili kusimamia ujenzi huo hadi ujenzi wa maabara ukamilike.

Akizungumza  kwenye kikao cha baraza la Madiwani kilichofanyika mjini Bagamoyo Mahiza alisema kuwa ujenzi wa maabara kwenye wilaya hiyo bado zoezi hilo haliko vizuri hivyo lazima itumike nguvu ya ziada kufanikisha zoezi hilo.

“Kuanzia sasa najua nitaanzia kata gani lakini nahamia Bagamoyo na wakuu wa idara kila mmoja tukitoka hapa ataniambia atakuwa kata gani ili tuanze usimamizi kwani bila ya kufanya hivi muda utaisha na mambo yatakuwa magumu,” alisema Mahiza.

“Kuanzia sasa vikao vya madiwani havitakuwepo kilichobaki wote tuende kwenye ujenzi wa maabara na kama mtu anaona hawezi kuwajibika aondoke mapema asije akatuharibia mipango yetu ya maendeleo kwani watoto ni wetu,” alisema Mahiza.

Mahiza alisema kuanzia sasa hivi hakuna cha mahafali wala sherehe wimbo uliopo ni maabara kwa shule zetu za sekondari kwani baadhi ndo wako kwenye msingi je ujenzi utakamilika kwa wakati jambo ambalo linatia mashaka.

“Baadhi ya watendaji hawana haraka na kusababisha shughuli kwenda taratibu kuanzia sasa hapa ni mwendo wa kufanya kazi kwani tusipokuwa makini muda utaisha hatujakamilisha itakuwa haipendezi,” alisema Mahiza.

Aidha alisema kuwa wakuu wa wilaya na mikoa waliitwa Dodoma na Rais na kutakiwa wawe wamekamilisha ujenzi huo ifikapo Novemba 30 mwaka huu na wao walimwahidi kuwa watakamilisha ujenzi kipindi hicho.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya Bagamoyo Shukuru Mbato alisema kuwa agizo hilo wamelipokea na watahakikisha wanakamilisha ujenzi wa maabara hizo kwa muda uliopangwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...