Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha Dorothy Mwanyika, akielezea uzoefu wa Tanzania katika eneo la Misaada Rasmi ya Maendeleo (ODA). Naibu Katibu Mkuu alikuwa mmoja wa wanajopo waliojadili mada kuhusu umuhimu wa ODA katika utekelezaji wa Malengo Maendeleo Endelevu baada ya 2015.
Sehemu ya washiriki wa mkutano ambao ni sehemu na maandalizi ya Mkutano wa Tatu wa Kimataifa kuhusu uwezeshwaji wa raslimali fedha kwa maendeleo endelevu baada ya 2015 mkutano unaotarajiwa kufanyika mapema mwakani huko Addis Ababa , Ethiopia, Naibu Katibu Mkuu Dorothy Mwanyika anaongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huu , ujumbe ambao umeshiriki kikamilifu katika majadiliano yanayoendelea hapa Umoja wa Mataifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...