MPANGO Taifa wa Damu Salama Tanzania (NBTS) unatoa rai kwa wananchi wote wenye sifa za kuchangia damu wajitokeze kuchangia damu katika vituo vya Damu salama hasa kipindi cha mwezi Novemba mpaka Januari mwakani , kipindi ambacho wanafunzi wa sekondari wanakuwa likizo hivyo kusababisha kuongezeka kwa uhaba wa damu nchini.

Hayo yalisemwa leo na Afisa Habari wa Mpango wa Taifa wa Damu Salama Tanzania Bw. Rajab Mwenda (pichani) katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika ilala mchikichini, Dar es salaam, alisema damu salama kwa kushirikiana na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na Chama cha Msalaba Mwekundu umekusanya chupa za damu asilimia 97% na kuvuka lengokatika kipindi cha miezi mitatu julai hadi septemba 2014.

Jumla ya chupa 40,974 zilikusanywa , lengo lilikuwa kukusanya chupa 42,500. \“Katika kipindi hicho chupa za damu zilizokusanywa toka vituo vidogo( Blood collection satellite sites) ni 2,886 (8%) ambapo kituo cha Morogoro chupa 1,158, Dodoma-818, M/moja-490, kigoma- 93 na Lindi-327)” alisema.

Alisema katika robo mwaka ya Julai- Septemba 2014 asilimia 32 ya jumla ya chupa zilizokusanywa zilitengenezwa mazao ya damu; Packed Red blood cell, chembe sahani (platelets) na plasma. Lengo lilikuwa ni kutengeneza 40% ya damu iliyokusanywa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...