Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Ngosi Mwihava (kushoto) akiagana na Balozi wa Australia nchini  anayemaliza muda wake, Geoff Tooth. 
 Balozi Geoff Tooth (kulia) akizungumza na Naibu Katibu Mkuu, Mhandisi Ngosi Mwihava ambapo Balozi huyo alimshukuru kwa ushirikiano alioupata kutoka katika Wizara na kumhakikishia kuwa Serikali ya Australia imedhamiria kuuenzi ushirikiano huo ambao ni wa kihistoria. Alisema Tanzania ijiandae na uwekezaji mkubwa kutoka kwa kampuni kubwa za Australia hususan katika masuala ya mafuta na gesi asilia.
Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati na Madini, Ngosi Mwihava (katikati) katika picha ya pamoja na Balozi Geoff Tooth (wa pili kutoka kulia). Wa kwanza kushoto ni Afisa wa wizara ya Mambo ya Nje katika Idara ya Asia na Australia, Bertha Makilagi, anayemfuatia ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Rasilimaliwatu Lusius Mwenda kutoka wizara ya Nishati na Madini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...