Kaimu Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa Benki ya NBC, Rukia Mtingwa (kushoto) akitoa elimu kuhusu ujasiriamali na baadhi ya vijana kutoka vyuoni walio katika kambi maalumu iliyoandaliwa na kampuni ya Maa Media kwa udhamini wa NBC mjini Bagamoyo, Pwani hivi karibuni. NBC ilitoa kiasi cha zaidi ya shs milioni 100 ambapo mbali na ujasiriamali vijana hao walifundishwa pia madhara na jinsi ya kuepuka matumizi ya madawa ya kulevya.
Meneja Huduma za Jamii wa NBC, Irene Peter (kulia), akisalimiana na Meneja Miradi wa Kampuni ya Maa Media, Albany James wakati yeye na Kaimu Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa benki hiyo, Rukia Mtingwa (kulia) walipotembelea kambi ya vijana iliyoandaliwa na Maa Media ili kuwafundisha masuala ya ujasiriamali, madhara na jinsi ya kuepukana na matumizi ya madawa ya kulevya. NBC ilitoa kiasi cha zaidi ya shs milioni 100 kwa ajili ya kambi hiyo iliyofanyika mjini Bagamoyo. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Lekoko Furaha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...