Lorietha Laurence -Maelezo.

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu , Joyce Fisoo  ametoa wito kwa kampuni za Filamu nchini kuwasilisha filamu zao ili ziweze kuhakikiwa na kulipiwa  kwa kupata kibali cha kuingia sokoni  kama sheria ya filamu ya mwaka 1976 kifungu namba 4 inavyoeleza.

Akizungumza  katika ofisi za Bodi leo jijini Dar es Salaam, Fisoo ameipongeza  kampuni ya Al-Riyamy Production  ambayo imeweza kutimiza wajibu wake na kulipia filamu 134 ambazo zimepata kibali cha kupatiwa stamp za  TRA na hivyo kuwa tayari kuingia sokoni. Aliongeza kuwa kuna baadhi za  kampuni za filamu nchini zimekiuka utaratibu na kushindwa kuwasilisha filamu zao kwa Bodi ikiwemo filamu zile zilizoigizwa  miaka ya zamani ambazo zimekuwa zikionyeshwa bila kibali.

 “Nimefurahishwa sana  kwa namna ambavyo kampuni ya Al-Riyamy  Production kwa kufuata sheria na kanuni za filamu nchini, hivyo natoa wito kwa kampuni nyingine pia kuweza kufanya  hivyo ili kukuza uchumi wetu na wao waweze kufanya biashara bila usumbufu” alisema Fisoo.

Naye mwakilishi wa kampuni ya Al- Riyamy Production Bakari Kassim almaarufu Mzee Jangala, amewaomba wasanii wenzake wenye kampuni za filamu waweze kufuata taratibu na sheria za bodi ya filamu ili kukuza soka la filamu na kuinua uchumi wa nchi yetu.

“Nawasiii wasanii wenzangu na wamiliki wa kampuni za filamu nchini waweze kufuata sheria na kanuni za filamu ili tuweze kwenda vizuri kwa kila mmoja kutimiza wajibu wake katika ulimwengu huu wa filamu” alisema Mzee Jangala. 

Baadhi ya kampuni ambazo zimeweza kuwasilisha kazi zao katika Bodi ya filamu ,ni pamoja na kampuni ya  Wananchi wote wamewasilisha filamu 119, Game First Quality filamu 35, steps Entertainment filamu 739, na Al-Riyamy Production  filamu 134.
 Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu , Joyce Fisoo  akiamwandikia kibali cha filamu mwakilishi wa kampuni ya Al- Riyamy Production Bakari Kassim almaarufu Mzee Jangala,(kulia) baada ya kufanya malipo ya filamu zao zote zikiwemo za zamani na mpya,leo jijini Dar es Salaam.
 Mwakilishi wa kampuni ya Al- Riyamy Production Bakari Kassim almaarufu Mzee Jangala,(kulia) akimuonyesha stakabadhi ya malipo Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu , Joyce Fisoo baada ya kufanya malipo ya kupata kibali kwa ajili ya filamu za kampuni hiyo,leo jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu , Joyce Fisoo  akimkabidhi kibali cha filamu mwakilishi wa kampuni ya Al- Riyamy Production Bakari Kassim almaarufu Mzee Jangala,(kulia) baada ya kufanya malipo ya filamu zao zote zikiwemo za zamani na mpya,leo jijini Dar es Salaam.
 Afisa Utamaduni wa Bodi ya Filamu Clarence Chelesi(kulia) akimpa mkono wa pongezi mwakilishi wa kampuni ya Al- Riyamy Production Bakari Kassim almaarufu Mzee Jangala,(kushoto) baada ya kupata kibali cha filamu,leo jijini Dar es Salaam.
Afisa Utamaduni wa Bodi ya Filamu Simon Peter (kulia)  akimpa mkono wa pongezi mwakilishi wa kampuni ya Al- Riyamy Production Bakari Kassim almaarufu Mzee Jangala,(kushoto) baada ya kupata kibali cha filamu wanaotazama ni Afisa Utamaduni wa Bodi ya Filamu Clarence Chelesi(katikati) na   Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu , Joyce Fisoo (kushoto) ,leo jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Lorietha Laurence-Maelezo).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Isiishie kuwasilishwa katika Bodi tu, pia hiyo Bodi ihakikishe filamu zinahakikiwa (edit) lugha iwe ni Kiswahili ama Kiingereza. Filamu zetu lugha ni ovyo sana (hasa tafasiri za Kiingereza). Ni aibu tupu, ukizingatia siku hizi zinaonekana katika baadhi ya chaneli za kimataifa!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...