Jeshi la Polisi leo limezuia mazishi ya aliyekuwa mnenguaji nguli wa bendi Aisha Mohammed Mbegu (Aisha Madinda) ili kujua mimi kilichosababisha kifo chake. 
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya The African Stars Entertainment (ASET) Bi. Asha Baraka amethibitisha hilo na kusema  kwamba mwili ndiyo ulikua unapelekwa Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi. 
“Mjomba wa marehemu amejaribu kuwaomba sana Polisi waache kuuchunguza mwili wa Aisha kwani wamemshukuru Mungu kwa yote lakini wamekataa hivyo hadi watakapomaliza kuchunguza ndipo watatupa mwili” alisema Asha.
Kifo cha Aisha ambacho kimejaa utata kutokana na jinsi kilivyotokea kwani hakuwa akiumwa na alikutwa amelala kibarazani kwa rafiki yake Samira Saleh huko Mabibo Jijini Dar es Salaam. 
Hata mtoto wake wa kiume Said alinukuliwa na kituo kimoja cha redio kwamba mwili wa mama yao ulipelekwa hospitali na mwanamke ambaye hata wao hawamfahamu na hapo ndipo panapoleta utata. Kifo cha Aisha kimethibishwa na Kamanda wa Kanda ya Polisi Mkoa wa Kinondoni Camillius Wambura. 
Juzi majira ya saa mbili asubuhi Aisha alikutwa na rafiki yake Samira Saleh akiwa amelala usingizi mzito kibarazani nyumbani kwake Mabibo (nyumbani kwa Samira). 
Marehemu Aisha anatarajiwa kuzikwa kesho  nyumbani kwao Mikadi Beach Kigamboni baada ya swala ya Ijumaa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. It is so sad, she is very young and full of life. Rest in peace

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...